Tuesday, April 16, 2013

Neno la leo

Zab 13:5-6 “Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. Naam, nimwimbie BWANA, kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu”

TAFAKARI: Kwa yale yote mema Mungu aliyokutendea, huna budi kumwimbia nyimbo na kumshukuru.Wapo watu wengine hawawezi kuomba msaada pale wanapokuwa na shida, lakini kutokana na wema wao Mungu hupendezwa nao na kuwaletea watu wa kuwasaidia bila wao kuomba msaada. Ni jambo la kumshukuru sana Mungu hasa kwa kutambua mengi aliyokutendea.
SALA: Mwenyezi Mungu, umekuwa mwema sana kwangu. Nakuamini wewe na yale ufanyayo katika maisha yangu. Saa nyingine naona kabisa uwepo wako na kufarijika moyoni mwangu. Naomba ukawaguse na wengine ambao bado hawajapitiwa na mkono wa upendo na ukarimu. Wapanguse machozi wanaolia Bwana, na uwape tumaini waliokata tamaa. Naomba na kupokea katika jina la Yesu, Amen.

No comments:

Post a Comment