Monday, April 15, 2013

Neno la leo

1Pet 1:13 “Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika Ufunuo wake Yesu Kristo”

TAFAKARI: Siku zote tunatakiwa kujiandaa kwa kitu chochote iwe vita, ama kazi ngumu ya aina yoyote. Labda mtu atafikiria natakiwa kufanya mazoezi ili niyakabili matakwa ya maisha ya kila siku, kitu ambacho si rahisi. Tunakiwa kujiandaa kiroho kwa kusoma neno la Mungu na kudumu katika imani, ili siku neema ikifunuliwa tuwe miongoni mwa wateule wa Mungu.
SALA: Bwana Mungu, nasoma neno lako kila siku na kufuata mafundisho yako, lakini Bwana nakiri kwamba mimi bado ni dhaifu. Wakati mwingine napatwa na matatizo na kujaribu kutatua shida hizo kwa akili zangu mwenyewe. Nisaidie Bwana nijiandae kiroho hata nikiteleza nisianguke pabaya, bali mikononi mwako. Naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment