Friday, April 12, 2013

Neno la leo

Rum 15:4 “Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini”

TAFAKARI: Maandiko matakatifu yameletwa wazi kwetu ili tutambue uzuri na ukuu wa Mungu. Lakini wengine hudiliki kulichanganua neno la Mungu na kusema halina maana, ukweli ji kwamba hawajazama ndani ya Kristo na kuelewa ukweli wa maandiko hayo. Kupitia neno lake watu wengi wamepokea miujiza.
SALA: Bwana Mungu, busara ya mafundisho yako katika neno lako inasema wazi jinsi maisha yangu yaliyobadilika. Naomba nisaidie niweze kudumu katika mafundisho yako ya Biblia, Bwana kwa maana nataka kuwa mwanafunzi wako wa kudumu na niweze kueneza neno la Upendo kupitia mafundisho hayo. Naomba kupitia Mwana wako Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment