Monday, April 8, 2013

Neno la leo

Mithali 16:9 “Moyo wa mtu huifikiri njia yake; bali BWANA huziongoza hatua zake”

TAFAKARI: Kwa kawaida mioyo yetu inabeba matumaini na mipango yetu ya baadae, lakini mwenye kujua muelekeo wa mipango hiyo ni Mungu pekee. Na mara nyingine tunashindwa kabisa kukamilisha mipango hiyo kwa wakati muafaka hivyo kukata tamaa. Lakini Mungu huwa upande wetu na kutupa nguvu mpya ya kuendelea.
SALA: Asante Mungu kwa kuniwezesha kukaa katika ulinzi wa mipango yako na si ya kwangu pekee. Mara nyingine mambo yanabadilika haraka na ninapoteza mwelekeo, lakini nikipiga hatua ya njia mpya najua unanibeba na kuniinua juu. Asante kwa kuniongoza katika njia nzuri kila siku. Katika jina la Yesu naomba na kushukuru, Amen.

No comments:

Post a Comment