Tuesday, April 9, 2013

Neno la leo

Ebr 1:1-2 “Mungu ambae alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu”

TAFAKARI: Mungu alikuwa na mpango mzuri wa mawasiliano tangu enzi za kale alipowatumia manabii wake. Anajua mambo ya zamani na hata ya baadae yatakayoikumba ulimwengu. Kwa kutambua hilo alimtoa mwanae wa pekee ambae kupitia yeye tutapata kuokolewa.
SALA: Mwenyezi Mungu ulijua ya kwamba watoto wako tunahitaji kusikia sauti yako hata ukapanga mawasiliano mema kati yetu na wewe. Wakati mwingine natamani kama ingekuwa rahisi kuwatambua manabii wako wengine. Lakini kwa kumtoa mwanao Yesu Kristo nimetambua uzuri wako, nimeona na umenijibu maombi yangu. Asante kwa kutoa mawasiliano yaliyo wazi kupitia nguvu za Mwana wako Yesu Kristo, kwa maana kupitia kwake yeye sisi tumepona.

No comments:

Post a Comment