Thursday, April 11, 2013

Neno la leo

Zab 23:5 “Waandaa meza mbele yangu, machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, na kikombe changu kinafurika"

TAFAKARI: Bwana Mungu huwakaribisha wale wote wamwendeao yeye. Pale mtu anapokutana na maadui wenye nia ya kumwangamiza, Yesu yuko pamoja naye chakulani akishibishwa neno la hekima, busara na ukweli.
SALA: Bwana Yesu nasema Asante kwa maana moyo wangu umejawa na Pendo lako kuu. Nikiwa na hofu juu ya adui zangu, nafikiria tu juu ya ulinzi wa nyumba yako ya milele na kujawa na nguvu mpya. Naomba unikinge zaidi dhidi ya maadui zangu na uniangazie nuru ya uso wako daima milele. Katika jina lako takatifu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment