Wednesday, April 10, 2013

Neno la leo

Wim 2:11-12 “Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake; Maua yatokea katika nchi, wakati wa kupelea umefika, na sauti ya mwigo husikiwa kwetu”

TAFAKARI: Kuna nyakati mtu hupitia misimu ya matatizo mbali mbali na mambo yake yote kuenda mlama. Pengine kwa kila ashikacho hubomoka ama huharibika kabisa. Lakini pindi mlango wa baraka ukifunguka kila kitu huenda sawa.
SALA: Bwana Mungu asante kwa kunionyesha matumaini pale nilipokata tamaa kabisa. Huu ni wakati wangu wa kufurahia matunda yako. Nakushukuru hata kwa mvua na mafuriko yaliyonipata, kwa maana yamenikuza na kunijenga kiakili na hata kuniletea baraka hizi sasa. Asante Mungu kwa upendo wako, Amen.

 

No comments:

Post a Comment