Friday, April 5, 2013

Neno la leo

1Yoh 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia”

TAFAKARI: Mungu husikia kila hitaji la mtu endapo tunamuomba kwa kuamini ya kwamba atatutimizia mahitaji yetu. Masikio yake yako wazi kusikia vilio vya mioyo yetu, hivyo hatuna budi kumuangalia yeye daima.
SALA: Bwana Mungu, asante kwa kunisikiliza. Natambua ya kwamba ni zawadi pekee kwa mimi kujiachia kwako Mungu kwa maana utaniondolea wasi wasi ndani ya moyo wangu. Mara nyingine nimekuwa na maswali ya ajabu na hata kuuliza juu ya mahitaji yangu, lakini wewe hukuacha kunisikiliza. Nakupenda Mungu wangu na kamwe sitaacha kukutumikia wewe. Katika jina Yesu naomba na kushukuru, Amen.

No comments:

Post a Comment