Thursday, April 4, 2013

Neno la leo

Zab 71:5 “Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu”

TAFAKARI: Ni jambo la faraja sana pale mtu anapompokea Kristo kuwa mwokozi wa maisha yake. Anakuwa mwenye nguvu mpya, mwenye wingi wa busara na hekima na zaidi Imani yake huongezeka maradufu kwa kumtegemea Mungu.
SALA: BWANA, nasema asante kwa nguvu unazonipa kila siku.Yale madirisha madogo ya bahati niliyokuwa nayo sasa yamekuwa milango mikubwa iliyo wazi. Kila kitu kiko sawa nikisimama kwa jina lako. Mungu naomba nizidishie imani hii ili nikadumu kwako daima milele. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment