Tuesday, April 2, 2013

Neno la leo

Wakolosai (Kol) 4:6 “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu anakosa maneno yenye busara wakati wa maongezi na wengine. Ama mtu anaweza akose kabisa maneno ya kumwambia mtu aliyefikwa na matatizo kama msiba ama matatizo ya aina yoyote ile. Yatupasa kumuomba Mungu atupe hekima na busara katika kuchagua maneno ya kuongea na wenzetu.

SALA: Bwana Mungu naomba unisaidie niguswe na pendo lako pale ninapotafuta maneno mazuri ya kusemezana na wenzangu. Naomba nipe hekima ya kuweza kutumia kinywa changu kuwabariki wengine nikiongozwa na roho wako mtakatifu. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment