Wednesday, April 17, 2013

Neno la leo

Zab 31:14 “Lakini mimi nakutumaini wewe, BWANA, Nimesema, wewe ndiwe Mungu wangu.

TAFAKARI: Tunapokiri kuwa Mungu wetu yupo basi tujaribu kufanya matendo yetu yaendane na kile tunachokiri. Tumuombe Mungu atusaidie kumkubali kwa nguvu bila kuona aibu.
SALA: Bwana Mungu, nataka midomo yangu ikuimbie wewe katika hali zozote, ziwe sherehe, misiba ama matatizo mengine, nataka mawazo yangu kwanza yawaze kukuimbia wewe na kukutukuza kwa sababu nakuamini wewe pekee katika maisha yangu. Naomba kila kitu nifanyacho kiwe ushuhuda wa kuamini kwangu. Nitasimama imara katika Imani niweze kutatua matatizo yangu. Naomba niwezeshe Bwana na usiniache kamwe. Naomba na kupokea katika jina la Yesu, Amen.

No comments:

Post a Comment