Wednesday, May 1, 2013

Neno la leo

1Pet 3:9 “Watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu akikosewa na mwingine hasira ikimpanda huweza kufanya maamuzi mabaya. Wengine huona kwamba mtu akimfanyia baya basi na yeye hulipiza baya. Maandiko yanatuasa kuishi kwa upendo, kuheshimiana na wenye kuhurumiana.

SALA: Bwana Mungu, mara nyingine nakuwa ni mtu wa kuweka kinyongo badala ya kuachia baraka pindi mtu anaponiudhi. Nahitaji msamaha wako Bwana na niponyeshe na hasira yangu hii ya haraka. Naomba nipe uwezo wa kuelewa utakatifu wako kabla kupatwa na tatizo lolote.Bwana haja yangu ni kurithi baraka zako kwa kueneza ukuu wa pendo lako kwetu. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment