Thursday, March 28, 2013

Neno la Leo

1 Yoh 1:7 “Bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote”

TAFAKARI: Tukimfuata Yesu, kamwe hatutakiwi kuyumba ama kupotea. Kwa kumfuata yeye, tunapata kutembea kwenye nuru wakati wa mchana na jioni hata mpaka anapotuongoza kwenye meza yake takatifu tushiriki chakula pamoja naye. Tunatakiwa tuendelee kuombeana na kufarijiana na hivyo tutazidi kung’ara hata kwenye giza na shetani hatopata nafasi kabisa.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba utuongoze tutembee kwenye nuru yako, na pia utuongoze kwenye meza yako takatifu tushiriki pamoja nawe chakulani siku zote za maisha yetu. Tunaomba na kupokea katika jina lako takatifu, Amen.

No comments:

Post a Comment