Monday, March 25, 2013

Neno la leo

Mk 6:55 “Wakaenda mbio wakizunguka nchi ile yote, wakaanza kuwachukua vitandani walio hawawezi, kwenda kila mahali waliposikia kwamba yupo”

TAFAKARI: Kwenye kipindi hiki cha kwaresma tumesoma habari zionyeshazo watu wakitembea kumfuata Yesu. Tumeona akiwaponya wagonjwa na kuwatangazia mateka uhuru juu ya kutekwa kwao, na hivyo kufanya habari zake njema kuenea kwa haraka. Vivyo hivyo hata tunapokaribia kumaliza kwaresma, yatupasa kuendelea kulieneza neno la Mungu na kuendeleza mwendo kasi wetu katika kutambua yale mazuri yatokanayo na neno lake.

SALA: Bwana Mungu, tunaomba utuwezeshe ili tuweze kukukimbilia wewe na zaidi tusaidie katika njia zote tupitazo ambazo zitatufanya tukufikie wewe. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment