Wednesday, March 27, 2013

Neno la Leo

Mathew 26:58 “Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya kuhani mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho”

TAFAKARI: Mara nyingine tunajificha tukidhani kwamba Yesu hatuoni. Ama tunaona aibu kujitambulisha kwamba sisi ni watoto wake yaani tunamtumikia Mungu pamoja na Yesu. Petro alijificha ili asikamatwe pamoja na Yesu kwenda kuteswa. Hii inatuonyesha kwamba, hata mmoja wa wafuasi wake wa karibu alimkana, lakini Yesu yeye hakumkana. Basi tudumu katika sala na kuomba neema ya msamaha na tuepukane na majaribu yaliko mbele yetu.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba utupe nguvu za kujiamini ili tuweze kutambulika pamoja nawe, na utupe mioyo iliyofunguka ili tufurahie uwepo wako uliopo ndani ya mioyo yetu. Katika jina lako takatifu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment