Tuesday, March 26, 2013

Neno la Leo

Mk 14:51 “Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata”

TAFAKARI: Hata yule mfuasi wa mwisho alipoacha kumfuata Yesu, tunaonyeshwa kijana mmoja ambaye hata jina halikufahamika yeye alikuwa anamfuata Yesu, naye akakamatwa kwenda kwenye hukumu ya kifo na Yesu. Tunakumbushwa kuwa upendo wa Yesu uko pale pale na kwa hadithi hii inatuwezesha kubaki ndani ya pendo hilo.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba nguvu ya kujiamini kwako na upendo wako vitualike tena ili tuweze tena kukufuata wewe kwenye ile njia ya hukumu ya kifo chako na hata pale utakaposhinda mauti. Katika jina lako takatifu tunaomba na kushukuru, Amen.

No comments:

Post a Comment