Friday, February 8, 2013

Neno la leo

Ebr 10:37-38 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”

TAFAKARI: Mngoje Bwana kwa matumaini makubwa kwa maana siku zi karibu kama anenavyo kwenye maandiko yake matakatifu. Kama utakuwa ni mtu mwenye imani haba, Mungu hatakuwa na furaha juu yako.
SALA: Mwenyezi Mungu nasema asante kwa maisha haya uliyonipa. Bwana naomba ukanizidishie imani ndani ya moyo wangu nikungoje wewe bila kuchoka, nijaze roho wako mtakatifu aliye msaidizi wa kila aliye mwaminifu ili imani yangu isitereleke. Naomba na kupokea katika jina la Yesu, Amen.

 

No comments:

Post a Comment