Monday, February 11, 2013

Neno la leo

Zab 107:20 “Hulituma neno lake, huwaponya, huwatoa katika maangaamizo yao”

TAFAKARI: Mungu ametuma neno lake ili litulishe, lituokoe, lituponye na kutushibisha kiroho.Mwamini yeye nawe utapata kuokolewa. 
SALA: Mwenyezi Mungu, nakushukuru kwa sababu, kwa kupitia neno lako nimepata neema ya msamaha, limeniokoa na nimeweza kudumu katika imani. Naomba uzidi kuniangalia mwanao na uzidi kuwa mponya kwa wale wanaokuamini. Jihidhihirishe kwa mataifa wasiokuamini wakapate kujua kwamba hakuna mkuu kama wewe. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment