Friday, February 15, 2013

Neno la leo

Isa 64:3 “Maana tangu zamani za kale watu hawakusikia, wala kufahamu kwa masikio, wala jicho halikuona Mungu, ila wewe atendaye mambo kwa ajili yake amngojaye”

TAFAKARI: Nyakati za sasa mambo mengi yanatokea na pengine tunajiuliza maswali mengi bila kupata majibu. Kuna wakati Mungu atashuka mwenyewe kwa ajili ya kuokoa kile kilichopotea. Muamini yeye na sikiliza neno lake udumu kiroho.
SALA: Bwana Mungu nimekukimbilia wewe nisiaibike milele, nimechagua kukusikiliza wewe siku zote za maisha yangu, hivyo nakuomba mkono wako wa rehema na uokoaji usinipungukie Bwana. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment