Thursday, February 14, 2013

Neno la leo

Yona 2:4 “Nami nikasema, nimetupwa mbali na macho yako; lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu”

TAFAKARI: Kuna kipindi mtu unajitenga na Mungu na kuwa mbali naye lakini kumbuka macho ya Bwana Mungu wetu yanaona kila mahali.
SALA: Asante Mungu kwa maana umeniokoa. Kuna wakati nilikuwa gizani Bwana lakini nilikutumaini wewe nikatazama hekalu lako na kujua ya kwamba bado hujanitupa mwana wako. Wewe usiyelala wala kusinzia naomba uzidi kuniangalia na kunitunza Mungu wangu, Katika jina la Yesu naomba na kushukuru Amen.

No comments:

Post a Comment