Thursday, February 7, 2013

Neno la leo

Gal 5:5 “Maana sisi wa roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani”

TAFAKARI: Pengine wewe ni mwenye imani haba, muombe Mungu akuongoze katika haki ili uweze kulifikia tumaini jema.Ukiwa unaamini hakika mambo yako mengi yatakuendea vyema. 
SALA: Niseme nini Bwana zaidi ya kushangaa makuu yako mengi,na umeniwezesha katika kufikia malengo yangu mengi. Bwana hata pale ninapokutana na vikwazo vingi, naomba uendelee kunipigania zaidi nikawe mwenye misimamo na kutokata tamaa.  Niimarishe katika kukuamini wewe Bwana kwa maana kwako tu ndo kuna tumaini jema.Naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment