Wednesday, February 6, 2013

Neno la leo

Ebr 4:13 “Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”

TAFAKARI: Hakuna kitu ambacho Mungu hawezi kuona kwa mwanadamu. Wakati mwingine mtu anaweza kutenda jambo la kikatili asijue ya kwamba Mungu anamuona, ila tambua ya kwamba Mungu anaona kila mahali.
SALA: Mungu baba, nakuja kwako kwa unyenyekevu nikiomba unisamehe dhambi nilizotenda ambazo machoni pa wanadamu hazifahamiki bali wewe wazitambua. Naomba uniweke huru kwa damu yako ya thamani, katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment