Tuesday, February 5, 2013

Neno la leo

Tito 2:11-12 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa”

TAFAKARI: Katika misemo ya kawaida kwa maisha yetu tunaposema kitu kumefunuliwa basi jua kina uwezo wa kufunikwa. Mungu ametoa neema kwa wanadamu wote kwa kutupa uhai na hivyo yatupasa kutenda mema, kwa maana ipo siku neema itafungwa na tumeshindwa kutimiza wajibu wetu kwa wakati tuliopewa hakika tutalia.

SALA: Mwenyezi Mungu asante kwa maana umenipa neema kuu machoni pangu. Nipe akili ya kutoweza kuichezea neema hii uliyonipa bure, niwezeshe katika muda wangu huu wa kuishi nikutumikie wewe daima.Naomba na kupokea katika jina la Kristo Yesu, Amen.

No comments:

Post a Comment