Monday, January 7, 2013

Zab 23:1-2 “Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza”

TAFAKARI: Ukiwa unamtegemea Mungu kamwe hautapungukiwa na kitu. Yeye ndiyo jibu la kila kitu na atakuweka mahali pazuri na kukukinga na mabaya.

SALA: Bwana Mungu, nakiri ya kwamba wewe ndiye mchungaji wangu na kamwe sitapungukiwa na kitu ukiwa nami.Umenitoa mbali na umeniongoza kwenye njia sahihi, sina budi kusema asante baba. Naomba unishike mkono Mungu wangu, nisirudi nyuma bali nikae kwako milele. Katika Jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.
Mbarikiwe!
 

1 comment: