Friday, January 11, 2013

Neno la leo

Waefeso 3: 20 “ Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuombayo au tuyawazayo, kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu”

TAFAKARI: Ama hakika hakuna mwenye ukuu kama Mungu. Yeye anaweza kukutendea mambo ya ajabu ambayo hata hujafikiria kwa akili zako ungeweza kuyafanya. Hutenda kwa wakati na pindi muda wake unapotimia hakuna awezaye kuzuia na hivyo hatuna budi kumtukuza yeye.

SALA: Mwenyezi Mungu, nasema asante kwa maana matendo yako yashangaza wengi. Nimeuona mkono wako wa baraka kwangu na ninaliinua jina lako na kulibariki milele. Utukuzwe daima na ninakuomba baba mkono wako wa baraka usinipungukie kamwe. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.
Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment