Thursday, January 10, 2013

Neno la leo

Zab 23: 6 “Hakika wema na fadhili zako zitanifuata, siku zote za maisha yangu. Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele,”
TAFAKARI: Yeye atuokoaye hawezi kutuacha wakiwa na wenye upungufu wa pendo lake. Ameahidi wema na fadhili zake zitakuwa pamoja nasi basi haina budi kukaa nyumbani mwake milele.
SALA: Mwenyezi Mungu nasema asante kwa maana nimeona mkono wako Bwana. Wewe ni mwenye wingi wa rehema, upendo na amani. Naomba wema wako na fadhili zako zinifuate siku zote na unitunze katika pendo lako. Zaidi nikiomba nidumu katika Imani na kukaa kwako daima. Katika jina la Yesu naomba na kushukuru, Amen.

 

No comments:

Post a Comment