Tuesday, January 8, 2013

Neno la leo

Zab 23: 3-4 “Hunihuisha nafsi yangu na kuniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami,gongo lako na fimbo yako vyanifariji”

TAFAKARI: Yeye Mungu anatuambia atatuongoza kwenye haki pale tunapoelekea pasipo. Atatukinga na mabaya kwa kutumia gongo lake na fimbo yake, hakuna lolote litakaloweza kupigana na hivyo.
SALA: Bwana Yesu asante kwa maana wewe umekuwa ngome yangu na msaada wangu kila nikuitapo. Wewe umesema utakuwa pamoja nami nipitapo katika bonde la uvuli wa mauti. Wewe uliyehuisha nafsi yangu naomba usiniache baba, siku zote za maisha yangu nikutumaini wewe. Katika jina la Yesu naomba nikipokea, Amen.

Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment