Monday, December 10, 2012

Neno la Leo

Zaburi 56:4 “Kwa msaada wa Mungu nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa, Mwenye mwili atanitenda nini”
Tafakari: - Mungu atusaidie kumwamini, kumtegemea na kumwogopa yeye siku zote za uhai wetu.
Sala:- Mwenyezi Mungu tunasema asante kwa kuwa wewe umekuwa kimbilio letu na ngome yetu kila tunapokuhitaji. Tunaomba uzidi kutuongoza na kutuimarisha katika neno lako siku zote tukaishi kwa kukutegemea wewe na kukuamini.  Tunaomba hayo kupitia mwanao mpendwa Yesu Kristo, mpatanishi na mwokozi wetu, Amen.
Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment