Wednesday, December 12, 2012

Neno la leo


Zab 133:1Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza; Ndugu wakae pamoja kwa umoja
Tafakari: Kama neno linavyosema Mungu anapendezewa na watu wakiishi pamoja kwa upendo na amani.Tunajua ya kwamba umoja ni nguvu na utengano ni dhaifu. Hivyo hatuna budi kushirikiana kwa kila jambo pale ambapo mwenzako, jirani ama ndugu yako anahitaji uwepo wako.
Sala: Mungu Baba, naomba uniepushe na ndimi zenye kuleta ugomvi, nipe moyo wa kupenda kushirikiana na jamaa zangu ili nikaishi kwa amani na jamii inizungukayo, na zaidi nikikuomba uimarishe upendo kati ya ndugu na ndugu. Naomba hayo kupitia Kristo Yesu, Amen.
Siku njema!
 

No comments:

Post a Comment