Thursday, December 13, 2012

Neno la leo

“Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa yako mabaki waliochaguliwa kwa neema. Lakini ikiwa ni kwa neema, haiwi kwa matendo tena au hapo neema isingekuwa neema.” Warumi 11:5-6
Tafakari: Matendo hayatuokoi bali neema hutuokoa. Mungu pekee ndiye atakayetuokoa na hivyo basi haina budi umkiri na kumwamini ndiyo wokovu unaingia halafu matendo yanafuata.
Sala: Mwenyezi Mungu, nasema asante kwa maana umeniokoa kwa damu ya thamani ya mwana wako Yesu Kristo. Naomba uyatawale maisha yangu, nielekeze katika kujua kuufanyia kazi wokovu wangu ili nipate neema yako. Naomba mapenzi yako yatimizwe katika hilo. Amen
Ubarikiwe!

 

No comments:

Post a Comment