Sunday, November 11, 2012

FUNGU LA KUMI/ THITHE


Fungu la kumi ni ile asilimia kumi ya mazao ama kipato cha mtu anachopata ambacho anatenga kwa ajili ya kumtolea Mungu.
Kwa kiingereza THITHE is the tenth part of agricultural produce or personal income set apart as an offering to God or for works of mercy, or the same amount regarded as an obligation or tax for the support of the church, priesthood, or the like. OR is a tenth part or any indefinitely small part of anything.
Asilimia 10 ya kipato chako unachotakiwa umtolee Mungu kinatakiwa kiwe kwenye gross salary na sio net salary. Katika hili wapo wenye mtazamo tofauti ya kwamba 10% inatoka kwenye net salary yaani baada ya makato. Binafsi mimi 10% yangu nahesabia kipato changu chote kabla ya makato. Natoa kwa moyo nikijua ya kuwa Mungu pekee ndo atanizidishia. Kumbuka ukitoa extra Mungu nae huona moyo wako ulivyo mkunjufu.
Watu wengi wanapatwa na vishawishi vya kuuliza pindi watoapo fungu lao la kumi ama sadaka zao kuwa zinaenda wapi. Epuka kishawishi cha namna hiyo kwa sababu kinakuzuia kupata baraka za Bwana. Kama utawala wa Kanisa utatumia fungu hilo la kumi kwa kufanya mambo yamchukizayo Mungu, ni juu ya yeye kuwahukumu. Mungu anakujua ya kwamba umemtolea na yeye atakubariki kwa sababu amependezwa na wewe. Kwa kujenga huu msingi wa utoaji fungu la kumi Mungu atakubariki kwenye masuala ya utajiri ambao ni mali, fedha, afya, usalama wako na mambo mengine yanayofanana na hayo. Kwa kifupi utauona mkono wa baraka wa Bwana katika nyanja mbali mbali za maisha yako. Mfano mzuri katika Biblia Kitabu cha Mwanzo 22 ni pale Ibrahimu alipomsikiliza Mungu pale alipotaka amtoe sadaka mwanae wa pekee Isaka. Alipotaka kufanya hivyo akasikia sauti ya Mungu ikimuasa asimtemdee mwanae hivyo kwa maana sasa amejua ya kuwa anamcha Mungu. Ule mstari wa 17 unasema “ katika kubariki nitakubariki na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni na kama mchanga ulioko pwani na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”
Jenga tabia ya kutoa kwa kuwa utoaji wako unampa Mungu heshima na utukufu. Ni sehemu kubwa ya utukufu. Mtolee Mungu kwa moyo wako wote na sio kutoka kana kwamba unamkopesha Mungu. 2Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala kwa lazima maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu”
Agano la kale linaonyesha kwamba watu walikuwa wakitoa mazao,na wanyama walionona kama fungu la kumi. Kwa ulimwengu wetu wa sasa ambapo watu wengi tumeajiriwa, fungu letu la kumi litahesabiwa kwenye kipato tupatacho katika kazi zetu ama biashara tufanyazo.
Katika kitabu cha Mithali 3:9 “Mheshimu BWANA kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote, ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.”
Pesa kwa sasa imekuwa ngumu na ndiyo maana watu wengine wana mitazamo tofauti ya fungu la kumi. Mtu mwingine anakuambia siwezi toa fungu la kumi kwa sababu sioni likizungumziwa kwenye Agano jipya. Lakini hii ni kutokana na ugumu wa utoaji na upofu wa mtu wa kujua ya kuwa ukimtolea Mungu kazi zako za mikono zinabarikiwa mara dufu. Na pili watu wamekuwa wakiiabudu sana pesa na kusahau kuwa Mungu huyo huyo ndo ametupa uweza wa kutawala vitu kama hivyo.
WAPI NATOA FUNGU LA KUMI
Malaki 3:10 “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo asema Bwana wa majeshi, mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha au la”
Toa fungu lako la kumi nyumbani kwa Bwana ambapo ni mahali unapokwenda kumwabudu yaani Kanisani. Kama umepanga kutoa fungu la kumi litoe hiyo siku uliyopanga, kwa kufanya kinyume chake utakuwa unamuibia Mungu. Kumuibia Mungu maana yake umepanga kutoa fungu lako la kumi kesho halafu inapofika siku ya kutoa unabadili mawazo ama kutoa fungu pungufu, hivyo ni kumuibia Mungu. Mtolee Mungu kwa wakati ulioahidi bila kukoma.
Ninavyoelewa kusaidia wajane, yatima, na wasiojiweza hiyo haihesabiwi kama fungu la kumi, bali inaingia katika upandaji mbegu, yaani kusaidia watu kwa moyo bila kusubiria mrejesho.Nasema hivyo kwa sababu wapo watu wanatoa msaada kwa yatima ama mtu asiyejiweza na kusema hili ndilo fungu langu la kumi. Mmoja wapo ni mimi nilikuwa nasema Mungu niongoze na nifunulie hii pesa nimpe nani ambaye anahitaji zaidi nikijua kuwa ni sehemu yangu ya fungu la kumi bila kujua nilikuwa namuibia Mungu. Kwa hiyo mtu aliyekuwa ananijia kichwani ndiyo nilikuwa nampelekea na kusema kwamba nimetoa fungu la kumi.

KUPANDA MBEGU
Pamoja na kutoa Fungu la kumi, ni vizuri kujenga tabia ya kupanda mbegu yaani kutoa fedha, msaada kwa watu mathalan yatima, wajane na wenye shida mbali mbali kwa nia ya kuvuna mema kutoka kwa Mungu. Kwa kifupi jenga tabia ya kusaidia watu lakini isiwe unafanya mfano kwamba unawekeana mkataba na Mungu ya kuwa ninamsaidia mtu fulani basi lazima Mungu aniongezee. Kwa kufanya hivyo hutafanikiwa kwa sababu unakuwa hujatoa kwa moyo wako wote. Mfano mzuri ni ule na Yesu na mpanzi ( Marko 4:3-8) aliyekwenda kupanda mbegu shambani mwake. Tena kuna hata na wimbo wake. “ Mpanzi alitoka kwenda panda mbegu njema shambani mwake, na nyingine zilianguka kwenye miiba, na nyingne zilianguka pakavu, na nyingine zilianguka kwenye udongo mzurii, zikazaa matunda zikimea na kukua, na kuzaa moja thelathini, moja sitini na moja mia”. Kwa kifupi panda mbegu yako kwenye udongo wenye rutuba, yaani saidia watu wale ambao unajua wanahitaji msaada zaidi kuliko kuwekeza katika miungu mingine.

Maandiko pia yanatuonyesha ya kwamba ni heri kutoa kuliko kupokea (Mdo 20:35). Kwa maana hiyo basi kwa pale unapotoa kwa watu usitegemee kurudishiwa kama ulivyotoa na pengine waweza usirudishiwe kabisa. Jua ya kuwa Mungu ndiyo mpaji, kwa kutoa kwako kwa moyo safi hakika utarudishiwa kwa namna nyingine. Mtolee Mungu kwa moyo wako wote hakika nawe utatimiziwa mahitaji yako. Waebrania 6:14 “Hakika yangu kubariki, nitakubariki na kuongeza nitakuongeza”

Where your treasure is, your heart will be!

 

No comments:

Post a Comment