Wednesday, November 14, 2012

Zaburi ya Leo

Zaburi 119: 41-48 "Ee Bwana, fadhili zako zinifikie na mimi, naam wokovu wako sawasawa na ahadi yako. Nami nitamjibu neno anilaumuye, kwa maana nalitumainia neno lako. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, maana nimezingojea hukumu zako. Nami nitaitii sheria yako daima, naam milele na milele. Nami nitakwenda panapo nafasi, kwa kuwa nimejifunza mausia yako. Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, wala sitaona aibu. Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako ambayo nimeyapenda. Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, nami nitazitafakari amri zako".
Muombe Mungu akupe fadhili zake na udumu katika neno lake. Kwa maana ni neno lake pekee litatuokoa. Songa mbele usisikilize watu wasemayo na siku zote mwanadamu hakosi la kusema. Iwe ni juu ya mafanikio yako ama jambo lolote bado kutakuwa na neno juu yake. Mtumainie Mungu na umuombe sana asiliondoe neno lake kinywani mwako. Zitafakari na kuzifuata amri zake hakika utaona uzuri wa kuishi kwa kumtegemea Mungu.

Mbarikiwe sana!

No comments:

Post a Comment