Thursday, November 15, 2012

Ujumbe wa leo


"Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu" Wafilipi 2:3-5
Mungu anakupenda ndiyo maana unaishi mpaka leo hii. Mungu wetu hapendezwi na majivuno wala kiburi hupendezwa na wale wenye unyenyekevu. Mungu anatuasa kuacha majivuno na kujiona ni bora kuliko mtu mwingine. Pia anasema tuache kushindana kwa lolote hususan yale tunayoshindania hayana baraka kwake wala hayajengi. Ubinafsi usichukue nafasi ndani ya mioyo yetu, hii itasababisha kututenga mbali na Mungu kwa maana mtu binafsi na mwenye kufanana na mambo kama hayo huhesabiwa maovu na baba yetu wa mbinguni.
Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment