Wednesday, November 7, 2012

Congrats Mr & Mrs John Adhero

"Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji ya mahali pakavu, nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako na baraka yangu juu yao utakaowazaa" Isaya44:3

Sote wanafamilia tumefurahi kupata habari hizi za ujio wa mgeni Brandon Willness Adhero. Hakika Mungu ni mwema na tutazidi kushangaa matendo yake kwetu sisi hasa ya uumbaji wake. Mungu awatunzie vijana wenu wakue katika misingi ya Kikristo. Awaongoze, awape busara na hekima katika kuwalea na kuwakuza Brandon na kaka yake Austin.
Nasi wanafamilia tunamuomba Mungu nae atuongoze kuwasaidia watoto hawa pale tuwezapo kimawazo katika hatua mbali mbali watakazopitia kimaisha mathalani katika kazi zao za shule na katika kukua kwao katika misingi ya Kristo wetu.
Bwana Mungu awaangazie nuru ya uso wake popote muendapo na katika lolote mfanyalo.
Brandon amezaliwa November 6, 2012!

1 comment:

  1. Thanks ma dear Sisy inlaw.... Me & ma family, we are so bless for the lovely msg. Thanks a lots! Brandon is doing go and mom too.

    ReplyDelete