Tuesday, May 28, 2013

Neno la leo


Zab 32:7 “Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso. Utanizungusha nyimbo za wokovu”

TAFAKARI: Nyakati ninazopatwa na uwoga huwa najificha. Na kuna wakati nawafwata marafiki ama jamaa ambao naona watanisaidia. Lakini najua wewe ndiye mwenye kuleta tumaini kuu.

SALA: Ee Bwana wangu, niokoe na upweke huu nilio nao kutokana na jambo hili linalonisumbua. Hukusema ya kwamba hautawapa majaribu wanao, kwa maana unatambua ya kwamba ni kupitia majaribu hayo unapima imani zetu juu yako.Nipe nguvu mpya niamke Bwana wangu na moyo wangu ukuimbie nyimbo za wokovu daima. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment