Wednesday, May 29, 2013

Neno la leo



Yak 1:4 “Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu anadhan amekabidhi tatizo lake kwa Mungu, lakini mtu huyo huanguka na kutenda dhambi. Yamkini ni kiburi, uzinzi, uongo, uchonganishi na mambo mengine yanayofanana na hayo. Mtu kama huyo ikiwa hajasimama imara basi kuna wepesi wa kuanguka na kutenda lile tatizo lake. Yatupasa kuomba Mungu atupe nguvu ya kujifunza saburi na kukaa kwake.

SALA: Bwana Mungu, wewe unashangaza kwa matendo yako makuu. Hata pale nilipokukosea, umeendelea kunitimizia mahitaji yangu na tena kwa wakati muafaka, kamwe sijapungukiwa na kitu. Naomba uzidi kufanya kazi ndani ya maisha yangu mpaka hapo ntakapokamilika kwa maana bado ni mchanga sana katika neno lako. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment