Friday, May 31, 2013

Neno la leo

Kumb 10: 12-13 “Na sasa, Israeli, BWANA, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda na kumtumikia BWANA, Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote; na kuzishika amri za BWANA na sheria zake anazokuamuru leo, upate uheri”

TAFAKARI: Jiulize mara ya mwisho ni lini umekaa ukazungumza na Mungu mambo kadhaa kutoka moyoni mwako? Pengine uko kwenye siku ya majonzi ama furaha, ama siku iliyofungamana na yote hayo. Biblia inatuasa kumpenda Mungu wetu ili tuishi kwa amani na tuwe wenye heri duniani.

SALA: BWANA, Mungu nashukuru kwa sababu uko katika maisha yangu. Asante kwa maana siku yangu inaenda kwa jinsi ulivyopanga wewe na nionapo uwepo wako kwangu nafarijika moyoni na kukumbuka ya kwamba ulishaahidi utatembea nami bega kwa bega popote niendapo. Naomba nizidishie moyo huu wa kuamini, kushukuru kuzishika amri zako BWANA. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment