Thursday, May 30, 2013

Neno la leo

Mit 31:17 “Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu”

TAFAKARI: Tumuombe Mungu atupe uwezo wa kuzama katika kutekeleza majukumu yetu iwe makazini ama nyumbani. Tuombe kuwa wafanyakazi hodari katika kila Nyanja lakini zaidi tukiweka mitazamo yetu kwake pekee.
SALA: Bwana Mungu, najua kila kitu kipo sawa na haki mbele ya macho yako. Naomba niongoze katika kufanya kazi ambazo unajua zina umuhimu kwako kwa maana nataka kazi zangu zikuridhishe na juu ya yote zinibariki. Naomba hata wakati nikilemewa na majukumu mengi, nisikusahau wewe Mungu bali niwe karibu nawe zaidi. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment