Friday, May 24, 2013

Neno la leo


Flp 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema”

TAFAKARI: Kusudi la Mungu katika maisha yetu ni jema. Mara nyingine ni vigumu kuelewa Mungu anataka nini kutoka kwetu sisi. Tumuombe Mungu atufanye tujue ya kwamba kusudi lake kuu hugusa imani ya wale wanaotuzunguka.

SALA: Mwenyezi Mungu, naomba ufanye kazi katika maisha yangu, nitumie Bwana vile upendavyo kwa maana najua una kusudi kubwa na mimi. Kuna wakati nilikuwa sielewi mambo yanayotokea kwenye maisha yangu, lakini sasa nimejua ya kwamba ulikuwa ukiniongoza kwenye kusudi lako kuu. Asante Bwana kwa kuwa naelewa kuna uzuri wa kusudi lako kuu kutimilika. Naomba hayo na kupokea katika jina la mwanao mpendwa wetu Yesu, Kristo anaeishi na kutawala daima milele, Amen.

No comments:

Post a Comment