Thursday, May 23, 2013

Neno la leo



Yak 4:4 “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu anafikiri anahitaji kufanya jambo fulani akubalike na ulimwengu. Chembe ya kutokujiamini hujiinua na kuona ni vyema afanye yale wengine wayafanyayo kwa kuwaridhisha wao. Tumwamini Mungu kwa maana yeye ndiye rafiki mkuu.

SALA: Bwana, nisamehe pale nilipochagua mambo ya dunia juu yako.Wewe umenifanyia mema sana mpaka nashindwa kuelewa kwanini naingia katika majaribu ya kufwata ya ulimwengu. Nisamehe Bwana,kwa kufuata vitu vya mpito wakati kwako wewe kuna utukufu mkuu. Naomba nirudishe kwako Bwana wangu, katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment