Monday, May 20, 2013

Neno la leo

Zab 38:15 “Kwa kuwa nakungoja wewe, BWANA, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu”

TAFAKARI: Kuwa na kiu ya Mungu ni jambo la kumpendeza sana. Na mtu akiwa kwenye hali hiyo hatataka kufanya maongezi ama kupata ushauri kutoka kwa marafiki. Kiu ya moyo wake ni kumuona Bwana kwa maana yeye ndiye mwenye upendo ulio kamili.
SALA: Bwana, mapigo ya moyo wangu yanaenda mbio nikisubiri uwepo wako kwangu. Nimekuita wewe katika nyakati zangu kuu za mahitaji na umejibu. Unanijua sana na kuona yaliyo ndani ya moyo wangu. Ee Bwana, asante kwa rehema zako, asante kwa kusikia vilio vyangu,asante kwa kunipenda jinsi hivi nilivyo, naomba univute kwenye ngome yako na unipe amani ya moyo. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment