Tuesday, May 21, 2013

Neno la leo

Ayu 16:20-21 “Rafiki zangu hunidharau, Lakini jicho langu humwagia Mungu machozi. Laiti angemtolea mtu hoja mbele ya Mungu, amtetee na mwanadamu mbele ya jirani yake”

TAFAKARI: Kuwa na rafiki anayemjua Mungu ipasavyo ni jambo la kumshukuru Mungu. Rafiki mzuri huombea rafiki zake, iwe ni wakati wa raha ama huzuni. Unaweza kupokea baraka kutokana na sala za wengine, hivyo usijidhanie nafsi yako kwa kusema ni kwa nguvu zako mwenyewe na sala zako.
SALA: Bwana, asante kwa maana najua umenipa rafiki anaeniombea. Mara nyingine nakuwa nimetingwa na uchovu wa kazi za kila siku na kujawa na hasira, lakini gafla napokea amani kutokana na juhudi za mwingine. Napatwa na faraja kubwa kujua ya kwamba rafiki yangu anasemezana na wewe juu yangu. Asante Bwana kwa sababu ya rafiki yangu na kwa kuwa sote tuna rafiki aliye wa kweli, ambaye ni wewe.

No comments:

Post a Comment