Monday, May 13, 2013

Neno la Leo

Mat 6:11 “Utupe leo riziki yetu”

TAFAKARI: Ni vyema tukatoa maisha yetu na kumpa Mungu kwa maana yeye hutoa vitu vingi tena vilivyo vikamilifu. Yeye ni mkate wetu wa maisha na kamwe hawezi kumuacha mtu na njaa.
SALA: Mwenyezi Mungu, wewe uliyenipa maisha na kunipatia kila hitaji langu la kila siku, naja mbele zako nikisema Asante. Pale nilipokuwa sina kitu katika maisha yangu, sasa nimekuwa na mengi ya kushukuru. Hata nitakaponung’unika kwa kuhitaji baraka zaidi, naomba nikumbushe kwamba riziki utoayo kila siku inatosha. Naomba kila iitwapo leo nikufurahishe wewe Mungu wangu. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea. Amen.

No comments:

Post a Comment