Friday, May 17, 2013

Neno la Leo

1Kor 14:12 “Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa”

TAFAKARI: Tumuombe Mungu zaidi kwa ajili ya karama za kiroho ili zitusaidie kuinua kanisa lake. Karama hizo ziwe zile zinazomtumikia Mungu kwa ajili ya utukufu wake, kwa maana tunatakiwa kuzirudisha kwakwe na kwa wale wanaomwamini.
SALA: Bwana Mungu, nipatie karama za kiroho ambazo zinakutumikia wewe. Hapo awali katika maisha yangu nilikuwa naomba kwa ajili ya karama zitakazonisaidia kufanikiwa katika maeneo mbali mbali kwneye maisha yangu, lakini sasa nimetambua ya kwamba nahitaji karama za kiroho zaidi. Pia naomba nipe maono ya kutambua karama za wengine ili niweze kuwa chachu ya kuwahimiza wao wakuone wewe katika mwili wa Kristo pekee. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

 

 

No comments:

Post a Comment