Tuesday, May 14, 2013

Neno la Leo

Habakuki 3:2 “Ee BWANA nimesikia habari zako, nami naogopa; Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka, Katikati ya miaka tangaza habari yake; katika ghadhabu kumbuka rehema”

TAFAKARI: “Waonyeshe Mungu” kuna wakati mtu hujikuta akipiga yowe ndani ya kichwa chake pale akiwa amezungukwa na watu wenye mioyo migumu wasioelewa maana ya maisha na kufanya mambo ya ajabu. Hufanya hivyo kwa mfano kama kwamba Mungu ni superman akimuita kuwaokoa, kutuokoa ama kuniokoa.
SALA: BWANA nakuja kwako nikijua wewe ni mwenye nguvu za ajabu, naomba uwaonyeshe watu hawa wasiojua pendo safi na wala msamaha. Badilisha mioyo ya wale walio na nia mbaya siku zote wako macho wazi kutaka kuwaumiza wengine. Ee BWANA sikia sala yangu hii leo, na zaidi nisaidie kuwaonyesha wewe na ukuu wako. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment