Thursday, May 16, 2013

Neno la leo

Rum 12:3 “Kwa maana Kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani”

TAFAKARI: Mara nyingine mtu hufanya mambo yake kwa kujitegemea mwenyewe na kujua ni kwa akili zake amefika mahali alipo. Lakini tunasahahu kwamba ni kwa Neema tu pekee tupo hapa tulipo sasa. Neema ya Bwana hutuweka huru kuwa wenyewe na vile vile kuturuhusu kumrudia Mungu. Tunapopata ukweli wa mambo katika maisha yetu ndipo tunagundua jinsi gani ni wadhaifu na kuanza kumlilia Mungu.
SALA: Bwana neema yako imeniwezesha kukurudia wewe, kuwa tegemezi kwako na mwenye moyo wa kushukuru. Asante Bwana kwa maana moyo wangu umejawa na pendo lako, naomba ya kuwa kila hatua ninayopiga iwe na muongozo kutoka kwako. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment