Friday, January 18, 2013

Neno la leo

Zab 37:7 “Ukae kimya mbele za Bwana, nawe umngojee kwa saburi. Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake, wala mtu afanyaye hila”

TAFAKARI: Mungu wetu hupenda wale wasikivu, wapole na wanyenyekevu mbele zake. Furahia maendeleo ya mwenzako na wala usimchukie mtu mwenye hila. Mngoje Bwana kwa saburi na hakika utamuona.
SALA: Mungu wangu na baba yangu, wewe uketiye mahali pa juu sana nakuomba unijalie hekima, busara na maarifa ili niwe na moyo wa kupenda wenzangu pale wafanikiwapo. Niondolee jicho la wivu ndani ya moyo wangu bwana, na unijaze roho wako mtakatifu ili nikaishi kwa kukutegemea wewe. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment