Tuesday, January 15, 2013

Neno la leo

Zab 145:17-18 “Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote. Bwana yu karibu na wote wamuitao,wote wamuitao kwa uaminifu”

TAFAKARI: Ukuu wa Mungu ni mkubwa katika kila atendalo nay eye hutimiza ahadi zake. Ni mwenye haki kwa kila kitu afanyacho na ni mwenye kujaa ukarimu wa pekee. Yeye yu karibu kwa wale wote wamtegemeao na kumuita kwa kwa kweli.
SALA: Mwenyezi Mungu, baba wa rehema nyingi na za ajabu machoni pangu, nakushukuru baba kwa maana umenifadhili mimi kwa kiasi kikubwa na umejibu maombi yangu. Naomba univute kwako niwe karibu nawe Bwana wangu na nikutumikie daima milele. Naomba hayo yote nikipokea, Amen.

No comments:

Post a Comment