Wednesday, January 16, 2013

Neno la leo

Zab 123: 1-2 “Nimekuinulia macho yangu wewe uketiye mbinguni. Kama vile macho ya watumishi kwa mkono wa bwana zao, kama macho ya mjakazi, kwa mkono wa bibi yake. Hivyo macho yetu humwelekea bwana, Mungu wetu, hata atakapoturehemu”

TAFAKARI: Siku zote tunamuangalia Bwana Mungu wetu ili tupate kubarikiwa. Yeye ni macho yetu, nuru yetu na nyota ituangaziayo wakati wa usiku na kutuongoza. Uwepo wake kwetu sisi ni upendo wa ajabu sana.
SALA: Bwana Mungu, nakuinulia macho yangu nikikuomba uwepo wako katika maisha yangu udumu. Wewe umekuwa msaada wangu usiniache kamwe bwana. Takasa njia zangu zote nipitazo na uniepushe na mitego ya muovu shetani. Naomba na kupokea katika jina la Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment