Thursday, January 17, 2013

Neno la leo

Zab 103:8 “Bwana amejaa huruma na neema, haoni hasira upesi,ni mwingi wa fadhili”

TAFAKARI: Mungu wetu ndiye anayeendesha maisha yetu na hakuna chochote kizuiacho nguvu zake za ukombozi kwetu sisi. Hata tunapokosa ama kuenenda katika njia zimchukizazo kwa maksudi kabisa, yeye huokoa nafsi zetu.
SALA: Mungu baba, wewe uliye mwepesi wa hasira nakuja mbele zako nikiomba msamaha kwa yale niliyokutenda. Bwana naomba unisaidie kuyasahau yale ya kale na uniongoze katika kukumbuka yale mambo ambayo yatanisaidia katika maisha ya yangu ya sasa na ya baadae. Nakupenda Bwana, naomba uwe ngome yangu milele, Amen.

No comments:

Post a Comment